Friday, May 8, 2015

Picha: Said Fella ampa zawadi ya gari kiongozi wa Yamoto Band, Aslay

[adsenseyu1]

 

Mkurugenzi wa kituo cha Mkubwa na Wanawe, Said Fella amempa zawadi ya gari kiongozi wa Yamoto Band Aslay Isihaka ambaye jana (May 7) alikuwa akisheherekea siku yake ya kuzaliwa.

Aslay
Fella akimkabidhi Aslay fungua za gari aliyomzawadia

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Fella alipost picha alipokuwa akimkabishi gari hiyo na kuandika ujumbe mrefu wa kumpongeza.

“MUNGU NDIO KILA KITU TATIZO MUDA NA SUBRA INSHAALLAH MWANETU ASLAY KITUO CHETU CHA MKUBWA NA WANAWE YOUTH CENTRE TEMEKE MIKOROSHINI TUNAJUA MCHANGO WAKO TANGU TUANZISHE KITUO IKI LEO TUMEONA WACHA TUKUZAWADIE NYEZO ILI MURADI IWE CHANGAMOTO KWA WENZAKO KITUONI APA KUONGEZA BIDII NA UPENDO NA KUJITOA KUSAIDIA WENZAO KAMA ULIVYO JITOA WEWE KWA WENZAKO INSHAALLAH MUNGU TUBARIKI SOTE SIE NA WADAU WETU PIA ATULINDIE AMANI YETU.baadaye tukutane matei jijini dodoma kwa burudani ya mkubwa na wanawe ya moto band njoo tucheze ngoma ya vijana mpya kimadoido.”

Aslay-2

Aslay naye alipost picha hiyo na ujumbe mrefu wa shukrani.

“Asante mungu Kwa kunipa uhai Na kipaji ambacho leo hii kina fanya naitwa Aslay pia nakushukuru kwa kunifikisha kwenye mikono Ya mtu mwenye moyo wa kibinaadamu. Najua kuna mengi makubwa ambayo boss wangu @mkubwafella umenifanyia ambayo si vyema kuyataja yote kwasababu wakati wake haujafikia ila naomba nichukue fulsa hii kukushukuru kwa hiki ulichonifanyia leo katika sherehe Ya kusherehekea siku yangu Ya kuzaliwa umenifanya nijione mwenye thamani kubwa duniani sikutegemea kama leo itakuwa siku yangu ya kumbukumbu ambayo sitoweza kuisahau hata Nije kuwa bilionea @mkubwafella asante kwa kunipa hii zawadi ambayo mimi kama mimi sikuiwazia kabisa kama Leo nitapata gari Na ninaushukuru uwongozi mziki Wa #mkubwanawanawe pamoja na manager wangu @chambusso boss wangu @babutale @mhtemba na mama yangu @sweatfella bila kuwasahau wasanii wenzangu wa @yamoto_band mungu ndie atakaewalipa … Nawatakia usiku mwema woote na Watu wa Dodoma Tukutane kesho pale Matei.”

0 comments:

Post a Comment