Showing posts with label zari. Show all posts
Showing posts with label zari. Show all posts

Friday, May 1, 2015

Zari: Watanzania wamenipokea kama mtu wao


[adsenseyu1]


Zari Tlale aka The Bosslady amesema upendo anaoupata baada ya kuanzisha uhusiano na Diamond Platnumz, umemfanya agundue kuwa watanzania wamemkubali kama mtu wao.







Akiongea na Clouds FM/TV asubuhi hii, Zari amesema tangu ameanza kuja Tanzania amekuwa akipokea upendo zaidi kutoka kwa watanzania kiasi ambacho kimemfanya ajisikie kama yupo kwao.

“Siwezi hata kulalamika, watu wa Tanzania ni wakarimu sana ni watu wazuri sana, kwangu mimi sijapata hata tatizo, siwezi hata kusema kitu chochote kibaya kuhusu watu wa Tanzania,” alisema.

“Wamenikaribisha kama ni mtu wao na sasa mimi ni wao hivyo ni yote ni heri kabisa,” aliongeza.

Katika hatua nyingine Zari amesema Tanzania itageuka kuwa makazi yake ya mara kwa mara na mipango iliyopo ni kuanzisha mradi wa kibiashara nchini lakini baada ya kufanya utafiti na kubaini fursa za uhakika.

“Siwezi tu nikafungua biashara hapa eti kwasababu mimi ni maarufu nikafungua tu biashara ya kijinga na nikidhani ninaweza nikauza wazo langu la kijinga kwa watu hapa, wao sio wajinga wanatumia hela zao hivyo nahitaji kubaini wapi kuna hitaji, kipi naweza kufanya na hapo ndipo ntaenda na kuwekeza fedha zangu.”


[adsenseyu2]


DIAMOND, ZARI WAFANYIWA EXCLUSIVE INTERVIEW CLOUDS TV/RADIO

Diamond na mpenzi wake Zari katika Exclusive One on One Interview ya Power Breakfast ya Clouds FM na 360 ya Clouds TV.

Diamond akimuweka sawa mpenzi wake.

Mtangazani mwenye jina kubwa wa Radio Clouds FM, Gerald Hando 'Mzee Mnoko' (kushoto) na Edson Kamoga wa 360 ya Clouds TV (kulia) wakiendelea kufanyia mahojiano Diamond na Zari.

Mtangazaji wa Clouds FM, Millard Ayo akisoma meseji za mashabiki waliokuwa wakifuatilia mahojiano hayo.

Baadhi ya wadau wa Clouds TV, Radio (kulia) wakipata kifungua kinywa kilichokuwa kimeandaliwa.



P Diamond na Zari wakiwa katika pozi na wadau wa Clouds TV, Radio baada ya mahojiano.

Wakati wakitoka.

Wadau wakiwa kwenye gari la Diamond wakati akijiandaa kuondoka mahali hapo.

(PICHA: MUSA MATEJA/GPL)